Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania

lbl_iso_certified

Kanda ya Kusini

Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania Kanda ya Kusini ipo Kusini mwa Tanzania ambayo inahudumia Mikoa mitatu (3); Mtwara, Lindi na Ruvuma. Ofisi za Kanda zipo katika Mkoa wa Mtwara. Kazi kubwa ya kanda ni kusimamia/kudhibiti Afya ya Mimea na viuatilifu katika Mikoa tajwa hapo juu.

                                                                                

Majukumu ya kanda ya Kusini:

  • Ukaguzi wa shehena za Mazao, Mimea Viuatilifu na bidhaa zingine za Kilimo zinazodhibitiwa na mamlaka zinazoingia na kutoka Nchini.
  • Kutoa vyeti vya usafi kwa mazao, mimea na bidhaa zitokanazo na mimea zinazosafirishwa kwenda nje ya Nchi
  • Ukaguzi wa maduka ya viuatilifu kwa wadau wa viuatilifu pamoja na kuwezesha usajili mpya kwa wafanyabiashara wa viuatilifu.
  • Ukaguzi wa maghala ya mazao na viuatilifu.
  • Kutoa mafunzo ya utambuzi na udhibiti wa visumbufu vya Mimea kwa mazao
  • Kutoa mafunzo ya matumizi sahihi na salama ya viuatilifu.
  • Ukaguzi wa mashamba maalumu ya mazao yanayosafirishwa kwenda nje ya Nchi.
  • Ukaguzi wa meli zinazoingia Nchini.
  • Uchunguzi na utabiri wa viashiria vya awali vya visumbufu vya mlipuko (Panya na Viwavi jeshi) katika maeneo yanayokabiliwa na visumbufu hivyo.

 

  • Vituo vya Ukaguzi vilivyopo Kanda ya Kusini:
  1. Bandari (Mtwara, Lindi, Kilwa- Lindi na Mbambabay- Ruvuma)
  2. Vituo vya mipakani (Mtambaswala- Mtwara, Kilambo- Mtwara, Chihanga- Mtwara na Mkenda- Ruvuma)
  3. Viwanja vya Ndege  (Mtwara na Songea)
  4. Ofisi za Posta (Mtwara, Lindi and Ruvuma)

 

Anuani ya Posta

TPHPA Kanda ya Kusini,
S.L.P 560,

Mtwara.

Barua pepe

mtwara@tphpa.go.tz